Zaburi 82

Zaburi 82

Zaburi 82

Maombi kwa ajili ya kutaka haki

1Mungu anaongoza kusanyiko kuu,

anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:

2“Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki

na kuonesha upendeleo kwa waovu?

3Teteeni wanyonge na yatima,

tunzeni haki za maskini na waliodhulumiwa.

4Mwokoeni mnyonge na mhitaji,

wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.

5“Hawajui lolote, hawaelewi lolote.

Wanatembea gizani;

misingi yote ya dunia imetikisika.

6“Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”;

ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’

7Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida;

mtaanguka kama mtawala mwingine yeyote.”

8Ee Mungu, inuka uihukumu nchi,

kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.