Zaburi 121

Hakikisho la ulinzi wa Mungu

1Nayainua macho yangu niitazame milima,

Msaada wangu utatoka wapi?

2Msaada wangu hutoka kwa BWANA,

Aliyezifanya mbingu na nchi.

3Hatauacha mguu wako usogezwe;[#1 Sam 2:9; Isa 27:3]

Akulindaye hatasinzia;

4Naam, hatasinzia wala hatalala,

Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5BWANA ndiye mlinzi wako;

BWANA ni uvuli katika mkono wako wa kulia.

6Jua halitakupiga mchana,[#Isa 49:10]

Wala mwezi wakati wa usiku.

7BWANA atakulinda na mabaya yote,[#Ayu 5:19; Zab 91:9,10; Mit 12:21]

Atakulinda nafsi yako.

8BWANA atakulinda utokapo na uingiapo,[#Kum 28:6; Mit 2:8]

Tangu sasa na hata milele.

The Holy Bible in Kiswahili, Revised Union Version © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 2013. 
Published by: Bible Society of Tanzania