Zaburi 131

Zaburi 131

Kumtumainia Mungu kwa utulivu

1Ee Mwenyezi-Mungu, sina moyo wa kiburi;

mimi si mtu wa majivuno.

Sijishughulishi na mambo makuu,

au yaliyo ya ajabu mno kwangu.

2Ila nafsi yangu imetulia na kuwa na amani,

kama mtoto mchanga alivyotulia na mama yake;

ndivyo nafsi yangu ilivyo tulivu.

3Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,

tangu sasa na hata milele.

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  
Published by: Bible Society of Tanzania