Zaburi 1

Zaburi 1

KITABU CHA KWANZA

Njia mbili

1Heri mtu yule asiyekwenda[#Mwa 5:24; Ayu 31:5; Zab 81:12; Mit 4:14]

Katika shauri la wasio haki;

Wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi;

Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo,

Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.

3Naye atakuwa kama mti uliopandwa[#Yer 17:8; Mwa 39:3; Zab 128:2]

Kandokando ya vijito vya maji,

Uzaao matunda yake kwa majira yake,

Wala jani lake halinyauki;

Na kila alitendalo litafanikiwa.

4Sivyo walivyo wasio haki;

Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

5Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni,

Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.

6Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki,[#Nah 1:7; Yn 10:14]

Bali njia ya wasio haki itapotea.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya