The chat will start when you send the first message.
1Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua,
Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
2Ee BWANA, Mungu wangu,[#Zab 6:2-4]
Nilikulilia ukaniponya.
3Umeniinua nafsi yangu,[#Zab 40:1,2]
Ee BWANA, kutoka kuzimu.
Umenihuisha na kunitoa
Miongoni mwao washukao Shimoni.
4Mwimbieni BWANA zaburi,
Enyi watauwa wake.
Na kutoa shukrani.
Kwa kukumbuka utakatifu wake.
5Maana ghadhabu zake ni za muda mfupi tu;[#Zab 16:11; Ufu 22:17]
Radhi yake ni ya milele.
Kilio huweza kuwapo usiku,
Lakini furaha huja asubuhi.
6Nami nilipofanikiwa nilisema,[#Ayu 29:18]
Sitaondoshwa milele.
7BWANA, kwa radhi yako[#Zab 104:29]
Wewe uliuimarisha mlima wangu.
Uliuficha uso wako,
Nami nikafadhaika.
8Ee BWANA, nilikulilia Wewe,
Naam, kwa BWANA niliomba dua.
9Mna faida gani katika damu yangu[#Zab 115:17]
Nishukapo Shimoni?
Mavumbi yatakusifu?
Yatautangaza uaminifu wako?
10Ee BWANA, usikie, unirehemu,[#Zab 4:1]
BWANA, uwe msaidizi wangu.
11Umegeuza msiba wangu kuwa ngoma;[#2 Sam 6:14]
Umeniondolea huzuni yangu, kunijalia furaha tele.
12Ili nafsi yangu ikusifu,
Wala isinyamaze.
Ee BWANA, Mungu wangu,
Nitakushukuru milele.