Zaburi 99

Zaburi 99

Sifa kwa utukufu wa Mungu

1BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka;[#Kut 25:22]

Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.

2BWANA ni mkuu katika Sayuni,

Naye ametukuka juu ya mataifa yote.

3Na walisifu jina lake kuu litishalo;[#Kum 28:58; Isa 6:3; Ufu 4:8]

Ndiye mtakatifu.

4Mfalme mkuu upendaye hukumu kwa haki;[#Kum 32:3,4; Ayu 36:5; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Mwa 18:25; #99:4 Katika Kiebrania ni nguvu za mfalme.]

Umeiimarisha haki;

Umefanya hukumu na haki katika Israeli.

5Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;[#1 Nya 28:2; Zab 132:7; Isa 66:1]

Sujuduni penye kiti cha miguu yake;

Ndiye mtakatifu.

6Musa na Haruni walikuwa makuhani wake,

Na Samweli pia ni miongoni mwa walioliitia jina lake,

Walimlilia BWANA naye akawaitikia;

7Akasema nao katika nguzo ya wingu.[#Kut 19:9; 33:9; Hes 12:5]

Wakashika shuhuda zake na amri aliyowapa.

8Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;[#Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20]

Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe

Ingawa uliwapatiliza matendo yao.

9Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;

Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu;

Maana BWANA, Mungu wetu, ni mtakatifu.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya