Zaburi 123

Zaburi 123

Kuomba huruma

1Nakutazamia kwa hamu, ee Mwenyezi-Mungu,

nakuangalia wewe utawalaye huko juu mbinguni!

2Kama watumishi wamtegemeavyo bwana wao,

kama mjakazi amtegemeavyo bibi yake,

ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe,

ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,

mpaka hapo utakapotuonea huruma.

3Utuhurumie, ee Mwenyezi-Mungu, utuhurumie,

maana tumedharauliwa kupita kiasi.

4Tumeshiba muda mrefu dharau za matajiri,

tumepuuzwa mno na wenye kiburi.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania