Zaburi 47

Zaburi 47

Mungu, Mfalme wa ulimwengu wote

1Enyi watu wote, pigeni makofi!

Msifuni Mungu kwa sauti za shangwe!

2Maana Mwenyezi-Mungu, Mungu Mkuu, anatisha.

Yeye ni Mfalme mkuu wa ulimwengu wote.

3Ametuwezesha kuwashinda watu wa mataifa,

ameyaweka mataifa chini ya mamlaka yetu.

4Ametuchagulia nchi hii iwe urithi wetu,

ambayo ni fahari ya Yakobo anayempenda.

5Mungu amepanda juu na vigelegele,

Mwenyezi-Mungu na sauti ya tarumbeta.

6Mwimbieni Mungu sifa, mwimbieni!

Mwimbieni mfalme wetu sifa, mwimbieni!

7Mwimbieni Mungu sifa kwa tenzi;

maana yeye ni mfalme wa ulimwengu wote.

8Mungu anayatawala mataifa yote;

amekaa katika kiti chake cha enzi kitakatifu.

9Viongozi wa watu wa mataifa wanakusanyika,

wanajiunga na watu wa Mungu wa Abrahamu,

maana nguvu zote duniani ni zake Mungu,

yeye ametukuka sana.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania