Zaburi 114

Zaburi 114

Zaburi 114

Maajabu ya Mwenyezi Mungu wakati Israeli walitoka Misri

1Israeli alipotoka Misri,

nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,

2Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,

Israeli akawa milki yake.

3Bahari ilitazama ikakimbia,

Yordani ulirudi nyuma,

4milima ilirukaruka kama kondoo dume,

vilima kama wana-kondoo.

5Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,

nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,

6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,

enyi vilima, kama wana-kondoo?

7Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,

mbele za Mungu wa Yakobo,

8aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,

mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.