Zaburi 23

Zaburi 23

Zaburi 23

Bwana mchungaji wetu

1Bwana ndiye mchungaji wangu,

sitapungukiwa na kitu.

2Hunilaza katika malisho

ya majani mabichi,

kando ya maji matulivu huniongoza,

3hunihuisha nafsi yangu.

Huniongoza katika njia za haki

kwa ajili ya jina lake.

4Hata nikipita katikati

ya bonde la uvuli wa mauti,

sitaogopa mabaya,

kwa maana wewe upo pamoja nami;

fimbo yako na mkongojo wako

vyanifariji.

5Waandaa meza mbele yangu

machoni pa adui zangu.

Umenipaka mafuta kichwani pangu,

kikombe changu kinafurika.

6Hakika wema na upendo vitanifuata

siku zote za maisha yangu,

nami nitakaa nyumbani mwa Bwana

milele.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.