Zaburi 3

Zaburi 3

Zaburi 3

Sala ya asubuhi ya kuomba msaada

1Ee Bwana , tazama adui zangu walivyo wengi!

Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!

2Wengi wanasema juu yangu,

“Mungu hatamwokoa.”

3Lakini wewe, Ee Bwana , ni ngao yangu pande zote;

umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.

4Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu,

naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.

5Ninajilaza na kupata usingizi;

naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.

6Sitaogopa makumi elfu ya adui,

wanaojipanga dhidi yangu kila upande.

7Ee Bwana , amka!

Niokoe, Ee Mungu wangu!

Wapige adui zangu wote kwenye taya,

vunja meno ya waovu.

8Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana .

Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.