Zaburi 32

Zaburi 32

Zaburi 32

Furaha ya msamaha

1Heri mtu aliyesamehewa makosa yake,

ambaye dhambi zake zimefunikwa.

2Heri mtu yule ambaye Bwana

hamhesabii dhambi,

na ambaye rohoni mwake

hamna udanganyifu.

3Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa

kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.

4Usiku na mchana

mkono wako ulinilemea,

nguvu zangu zilinyonywa

kama vile katika joto la kiangazi.

5Kisha nikakiri dhambi yangu kwako,

wala sikuficha uovu wangu.

Nilisema, “Nitaungama

makosa yangu kwa Bwana .”

Ndipo uliponisamehe

hatia ya dhambi yangu.

6Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe

wakati unapopatikana,

hakika maji makuu yatakapofurika

hayatamfikia yeye.

7Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha,

utaniepusha na taabu

na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.

8Nitakufundisha na kukuonesha njia utakayoiendea;

nitakushauri na kukuangalia.

9Usiwe kama farasi au nyumbu

wasio na akili,

ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu

la sivyo hawatakukaribia.

10Mtu mwovu ana taabu nyingi,

bali upendo usio na kikomo wa Bwana

unamzunguka mtu anayemtumaini.

11Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki!

Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.