Zaburi 123

Zaburi 123

Ombi la huruma

1Nimekuinulia macho yangu,

Wewe uketiye mbinguni.

2Kama vile macho ya watumishi

Yanavyoutegemea mkono wa bwana zao

Kama macho ya mjakazi

Yanavyoutegemea mkono wa bibi yake;

Ndivyo macho yetu yanavyomtegemea BWANA, Mungu wetu,

Hadi atakapoturehemu.

3Uturehemu, Ee BWANA, uturehemu sisi,

Kwa maana tumeshiba dharau.

4Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha,

Na dharau ya wenye kiburi.

The Holy Bible in Kiswahili, Revised Union Version © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 2013. 
Published by: Bible Society of Tanzania