Zaburi 4

Zaburi 4

Ombi la kuokolewa kutoka kwa adui

1Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo;

Uliniokoa nilipokuwa katika shida;

Unifadhili na kuisikia sala yangu.

2Enyi wanadamu, hadi lini utukufu wangu utafedheheka?

Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo hadi lini?

3Bali jueni ya kuwa BWANA amejiteulia mtauwa;[#Kut 33:16; 2 Pet 2:9]

BWANA husikia nimwitapo.

4Muwe na hofu wala msitende dhambi,[#Efe 4:26; Mit 3:7]

Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.

5Toeni dhabihu za haki,[#Kum 33:19; Zab 37:3]

Na kumtumaini BWANA.

6Wengi husema, Nani atakayetuonesha mema?[#Zab 80:3]

BWANA, utuinulie nuru ya uso wako.

7Umenitia furaha moyoni mwangu,

Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai.

8Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara,[#Law 26:5; Kum 12:10; Yn 14:27; Flp 4:7]

Maana Wewe, BWANA, peke yako,

Ndiwe unijaliaye kukaa salama.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya