Zaburi 127

Zaburi 127

Bila Mungu kazi ya binadamu haifai

1Mwenyezi-Mungu asipoijenga nyumba,

waijengao wanajisumbua bure.

Mwenyezi-Mungu asipoulinda mji,

waulindao wanakesha bure.

2Mnajisumbua bure kuamka mapema asubuhi

na kuchelewa kwenda kupumzika jioni,

mjipatie chakula kwa jasho lenu.

Mungu huwaruzuku walio wake hata walalapo.

3Watoto ni riziki kutoka kwa Mwenyezi-Mungu;

watoto ni tuzo lake kwetu sisi.

4Watoto waliozaliwa wazazi wakiwa bado vijana,

ni kama mishale mikononi mwa askari.

5Heri mtu aliye na mishale hiyo kwa wingi.

Hatashindwa atakapokabiliana na adui mahakamani.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania