The chat will start when you send the first message.
1Heri mtu anayewajali maskini;
Mwenyezi-Mungu atamwokoa wakati wa shida.
2Mwenyezi-Mungu atamlinda na kumweka hai,
naye atafanikiwa katika nchi;
Mungu hatamwacha makuchani mwa maadui zake.
3Mwenyezi-Mungu atamsaidia awapo mgonjwa,
atamponya maradhi yake yote.
4Nami nilisema: “Unifadhili, ee Mwenyezi-Mungu,
unihurumie maana nimekukosea wewe.”
5Madui zangu husema vibaya juu yangu:
“Atakufa lini na jina lake litoweke!”
6Wanitembeleapo husema maneno matupu;
wanakusanya mabaya juu yangu,
na wafikapo nje huwatangazia wengine.
7Wote wanichukiao hunongonezana juu yangu;
wananiwazia mabaya ya kunidhuru.
8Husema: “Maradhi haya yatamuua;
hatatoka tena kitandani mwake!”
9Hata rafiki yangu wa moyoni niliyemwamini,[#Taz Mat 26:23; Marko 14:18; Luka 22:21; Yoh 13:18]
rafiki ambaye alishiriki chakula changu,
amegeuka kunishambulia!
10Ee Mwenyezi-Mungu, unionee huruma!
Unipe nafuu, nami nitawalipiza.
11Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami,
maadui zangu wasipopata fahari juu yangu.
12Wewe umenitegemeza kwani natenda mema;
waniweka mbele yako milele.
13Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,[#Taz Zab 106:48]
tangu milele na hata milele!