Zaburi 127

Zaburi 127

Zaburi 127

Bila Mwenyezi Mungu, kazi ya mwanadamu haifai

1Mwenyezi Mungu asipoijenga nyumba,

wajengao hufanya kazi bure.

Mwenyezi Mungu asipoulinda mji,

walinzi wakesha bure.

2Mnajisumbua bure kuamka mapema

na kuchelewa kulala,

mkitaabikia chakula:

kwa maana yeye huwapa usingizi wapendwa wake.

3Watoto ni urithi unaotoka kwa Mwenyezi Mungu,

uzao ni zawadi kutoka kwake.

4Kama mishale mikononi mwa shujaa

ndivyo walivyo wana awazaao mtu katika ujana wake.

5Heri mtu ambaye podo lake

limejazwa nao.

Hawataaibishwa wanaposhindana

na adui zao langoni.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.