Zaburi 128

Zaburi 128

Zaburi 128

Thawabu ya kumtii Mwenyezi Mungu

1Heri wale wote wamchao Mwenyezi Mungu,

wanaoenda katika njia zake.

2Utakula matunda ya kazi yako;

baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

3Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao

ndani ya nyumba yako;

wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni

kuizunguka meza yako.

4Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchaye Mwenyezi Mungu.

5Mwenyezi Mungu na akubariki kutoka Sayuni

siku zote za maisha yako,

na uone mafanikio ya Yerusalemu,

6nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.

Amani iwe juu ya Israeli.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.