Zaburi 70

Zaburi 70

Zaburi 70

Kuomba msaada

(Za 40:13‑17)

1Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa;

Ee Bwana , njoo hima unisaidie.

2Wale wanaotafuta kuniua,

waaibishwe na kufadhaishwa;

wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,

warudishwe nyuma kwa aibu.

3Wale wanaoniambia, “Aha! Aha!”

na warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

4Lakini wote wanaokutafuta

washangilie na kukufurahia,

wale wanaoupenda wokovu wako siku zote waseme,

“Bwana ni mkuu!”

5Lakini mimi bado ni maskini na mhitaji;

Ee Mungu, unijie haraka.

Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;

Ee Bwana , usikawie.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.