Zaburi 8

Zaburi 8

Zaburi 8

Utukufu wa Mungu na heshima ya mwanadamu

1Ee Bwana , Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani kote!

Umeuweka utukufu wako

juu ya mbingu.

2Midomoni mwa watoto wachanga na wanaonyonya

umeamuru sifa,

kwa sababu ya watesi wako,

kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi.

3Nikiziangalia mbingu zako,

kazi ya vidole vyako,

mwezi na nyota,

ulizoziratibisha,

4mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,

binadamu ni nani hata unamjali?

5Umemfanya chini kidogo kuliko viumbe wa mbinguni,

ukamvika taji la utukufu na heshima.

6Umemfanya mtawala juu ya kazi za mikono yako;

umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.

7Mifugo na makundi yote pia,

naam, na wanyama wa kondeni,

8ndege wa angani na samaki wa baharini,

naam, kila kinachoogelea katika njia za bahari.

9Ee Bwana , Bwana wetu,

tazama jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani kote!

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.