Zaburi 113

Zaburi 113

Sifa kwa Mungu mtukufu

1Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Enyi watumishi wa Mwenyezi-Mungu, lisifuni jina lake!

2Jina lake litukuzwe,

sasa na hata milele.

3Kutoka mashariki na hata magharibi,

litukuzwe jina la Mwenyezi-Mungu!

4Mwenyezi-Mungu atawala juu ya mataifa yote,

utukufu wake wafika juu ya mbingu.

5Nani aliye kama Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu?

Yeye ameketi juu kabisa;

6lakini anatazama chini,

azione mbingu na dunia.

7Humwinua fukara kutoka mavumbini;

humnyanyua maskini kutoka unyonge wake,

8na kumweka pamoja na wakuu;

pamoja na wakuu wa watu wake.

9Humjalia mwanamke tasa furaha nyumbani kwake;

humfurahisha kwa kumjalia watoto.

Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania