Zaburi 124

Zaburi 124

Mungu kinga yetu

1“Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu

Semeni nyote mlio katika Israeli:

2“Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu,

wakati ule tuliposhambuliwa na maadui,

3hakika tungalimezwa tukiwa hai,

wakati hasira zao zilipotuwakia.

4Tungalikumbwa na gharika,

tungalifunikwa na mto wa maji,

5mkondo wa maji ungalituchukua!”

6Atukuzwe Mwenyezi-Mungu,

ambaye hakutuacha makuchani mwao.

7Tumeponyoka kama ndege mtegoni;

mtego umeteguliwa, nasi tukaokoka.

8Msaada wetu watoka kwa Mwenyezi-Mungu,

aliyeumba mbingu na dunia.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania