Zaburi 150

Zaburi 150

Zaburi ya kumsifu Mungu

1Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Msifuni Mungu katika patakatifu pake;

msifuni katika mbingu zake kuu.

2Msifuni kwa sababu ya matendo yake makuu;

msifuni kwa ajili ya utukufu wake mkuu.

3Msifuni kwa mlio wa tarumbeta;

msifuni kwa zeze na kinubi!

4Msifuni kwa ngoma na kucheza;

msifuni kwa filimbi na banjo!

5Msifuni kwa kupiga matoazi.

Msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa.

6Kila kiumbe hai kimsifu Mwenyezi-Mungu!

Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania