Zaburi 128

Zaburi 128

Tuzo kwa jamaa imchayo Mungu

1Heri wote wamchao Mwenyezi-Mungu,

wanaoishi kufuatana na amri zake.

2Utapata matunda ya jasho lako,

utafurahi na kupata fanaka.

3Mkeo atakuwa kama mzabibu wa matunda mengi nyumbani mwako;

watoto wako kama chipukizi za mzeituni kuzunguka meza yako.

4Naam, ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchaye Mwenyezi-Mungu.

5Mwenyezi-Mungu akubariki kutoka Siyoni!

Uione fanaka ya Yerusalemu, siku zote za maisha yako.

6Uishi na hata uwaone wajukuu zako!

Amani iwe na Israeli!

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania