Zaburi 100

Zaburi 100

Zaburi 100

Dunia yote yaitwa kumsifu Mwenyezi Mungu

1Mpigieni Mwenyezi Mungu kelele za shangwe, dunia yote.

2Mwabuduni Mwenyezi Mungu kwa furaha;

njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.

3Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Mungu.

Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake;

sisi tu watu wake,

kondoo wa malisho yake.

4Ingieni malangoni mwake kwa shukrani

na katika nyua zake kwa kusifu,

mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.

5Kwa maana Mwenyezi Mungu ni mwema

na fadhili zake zadumu milele;

uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.