Zaburi 11

Zaburi 11

Zaburi 11

Kumtumaini Bwana

1Kwa Bwana ninakimbilia.

Unawezaje basi kuniambia:

“Ruka kama ndege utorokee kwenye mlima wako.

2Hebu tazama, waovu wanapinda nyuta zao;

wanaweka mishale kwenye nyuzi zake

ili wakiwa gizani, wawapige

walio wanyofu wa moyo.

3Wakati misingi imeharibiwa,

mwenye haki anaweza kufanya nini?”

4Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu;

Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.

Huwaangalia wana wa watu,

macho yake yanawachunguza.

5Bwana huwachunguza wenye haki,

lakini nafsi yake inachukia waovu

na wale wanaopenda mapigano.

6Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali

na kiberiti kinachowaka;

upepo wenye joto kali ndio fungu lao.

7Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki,

yeye hupenda haki.

Wanyofu watauona uso wake.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.