Zaburi 12

Zaburi 12

Zaburi 12

Kuomba msaada

1Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;

waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.

2Kila mmoja humwambia jirani yake uongo;

midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.

3Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila

na kila ulimi uliojaa majivuno,

4ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda;

midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”

5“Kwa sababu wanyonge wanaonewa,

na wahitaji wanalia kwa uchungu,

nitainuka sasa,” asema Bwana .

“Nitawalinda kutokana na wale

wenye nia mbaya juu yao.”

6Maneno ya Bwana ni safi,

kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,

iliyosafishwa mara saba.

7Ee Bwana , utatuweka salama

na kutulinda na kizazi hiki milele.

8Watu waovu huenda wakiringa kila mahali

wakati yule aliye mbaya sana

ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.