Zaburi 137

Zaburi 137

Zaburi 137

Maombolezo ya Israeli uhamishoni

1Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza

tulipokumbuka Sayuni.

2Kwenye miti ya huko

tulitundika vinubi vyetu,

3kwa maana huko hao waliotuteka

walitaka tuwaimbie nyimbo;

watesi wetu walidai nyimbo za furaha;

walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja

kati ya nyimbo za Sayuni!”

4Tutaimbaje nyimbo za Mwenyezi Mungu,

tukiwa nchi ya kigeni?

5Nikikusahau wewe, ee Yerusalemu,

basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.

6Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu

kama sitakukumbuka wewe,

kama nisipokufikiri Yerusalemu

kuwa furaha yangu kubwa.

7Kumbuka, Ee Mwenyezi Mungu, walichokifanya Waedomu,

siku ile Yerusalemu ilipoanguka.

Walisema, “Bomoa, bomoa

hata misingi yake!”

8Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa,

heri yeye atakayekulipiza wewe

kwa yale uliyotutenda sisi:

9yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga

na kuwaponda juu ya miamba.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.