Zaburi 14

Zaburi 14

Zaburi 14

Uovu wa wanadamu

(Za 53)

1Mpumbavu anasema moyoni mwake,

“Hakuna Mungu.”

Wamepotoka, matendo yao ni maovu kabisa;

hakuna hata mmoja atendaye mema.

2Bwana anawachungulia wanadamu

kutoka mbinguni

aone kama kuna mwenye hekima,

yeyote anayemtafuta Mungu.

3Wote wamepotoka,

wote wameoza pamoja;

hakuna atendaye mema,

naam, hakuna hata mmoja!

4Je, watendao maovu kamwe hawatajifunza:

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

hao ambao hawamwiti Bwana ?

5Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu,

maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.

6Ninyi watenda maovu mnakwamisha mipango ya maskini,

bali Bwana ndiye kimbilio lao.

7Laiti wokovu wa Israeli

ungekuja kutoka Sayuni!

Bwana anaporejesha

wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie,

Israeli na afurahi!

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.