Zaburi 15

Zaburi 15

Zaburi 15

Kitu Mwenyezi Mungu anachotaka

1Mwenyezi Mungu, ni nani awezaye kukaa

katika Hekalu lako?

Nani awezaye kuishi

katika mlima wako mtakatifu?

2Ni yule aendaye pasipo mawaa,

atendaye yaliyo haki,

asemaye kweli toka moyoni mwake,

3na hana masingizio ulimini mwake,

asiyemtenda jirani yake vibaya,

na asiyemsingizia mwenzake,

4ambaye humdharau mtu mbaya,

lakini huwaheshimu wale wamwogopao Mwenyezi Mungu,

yule atunzaye kiapo chake

hata kama anaumia.

5Yeye akopeshaye fedha yake bila riba,

na hapokei rushwa dhidi ya mtu asiye na hatia.

Mtu afanyaye haya

kamwe hatatikisika.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.