Zaburi 36

Zaburi 36

Zaburi 36

Uovu wa mwanadamu

1Kuna neno moyoni mwangu

kutoka kwa Mungu

kuhusu hali ya dhambi ya mwovu.

Hakuna hofu ya Mungu

mbele ya macho yake.

2Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno

hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.

3Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu,

ameacha kuwa mwenye hekima au kutenda mema.

4Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya,

hujitia katika njia ya dhambi

na hakatai lililo baya.

5Upendo wako, Ee Bwana , unafika hadi mbinguni,

uaminifu wako hadi kwenye anga.

6Haki yako ni kama milima mikubwa,

hukumu zako ni kama kilindi kikuu.

Ee Bwana , wewe huwahifadhi

mwanadamu na mnyama.

7Upendo wako usiokoma

ni wa thamani mno!

Watu wakuu na wadogo

hujificha uvulini wa mabawa yako.

8Wanajifurahisha katika wingi ulio nyumbani mwako,

nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.

9Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima,

katika nuru yako twaona nuru.

10Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe,

haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.

11Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu,

wala mkono wa mwovu usinifukuze.

12Tazama jinsi watenda maovu walivyoanguka:

wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.