Zaburi 57

Zaburi 57

Zaburi 57

Kuomba msaada

1Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie,

kwa maana nafsi yangu inakukimbilia.

Chini ya uvuli wa mabawa yako nitakimbilia

hadi maafa yapite.

2Namlilia Mungu Aliye Juu Sana,

Mungu anayetimiza makusudi yake kwangu.

3Hutumana msaada kutoka mbinguni na kuniokoa,

akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali;

Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.

4Niko katikati ya simba;

nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kali,

watu ambao meno yao ni mikuki na mishale,

ambao ndimi zao ni panga kali.

5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

utukufu wako na uenee duniani kote.

6Waliitegea miguu yangu nyavu,

nikachoshwa na dhiki.

Wamechimba shimo katika njia yangu,

lakini wametumbukia humo wao wenyewe.

7Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti,

moyo wangu ni thabiti;

nitaimba na kusifu kwa nyimbo.

8Amka, nafsi yangu!

Amka, kinubi na zeze!

Nitayaamsha mapambazuko.

9Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kati ya mataifa;

nitaimba habari zako, kati ya jamaa za watu.

10Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni,

uaminifu wako unazifikia anga.

11Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni,

utukufu wako na uwe duniani pote.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.