Yesaya 4

Yesaya 4

1Siku ile wake saba watamshika mume mmoja na kumwambia:

Tutajipatia wenyewe vilaji na mavazi,

tunataka tu kuitwa kwa jina lako, utuondolee soni zetu!

Wokovu utakaotokea Yerusalemu.

2Siku ile mche wa Bwana

utakuwa wenye urembo na macheo,

nao uzao wa nchi

utakuwa wenye ukuu na utukufu

kwao Waisiraeli waliopona.

3Atakayekuwa amebakizwa Sioni,

naye atakayekuwa amesazwa Yerusalemu ataitwa mtakatifu,

ni kila mmoja wao aliyeandikiwa kuwapo Yerusalemu.

4Hapo ndipo, Bwana atakapokuwa amekwisha kuyaosha

machafu yao wanawali wa Sioni,

napo ndipo, atakapokuwa amekwisha kuzitowesha mwao

damu zilizomwagwa Yerusalemu;

atavifanya kwa nguvu za roho yenye mapatilizo

na kwa nguvu za roho yenye moto.

5Kwenye makao yote ya mlimani kwa Sioni

nako kwenye makutano ya kumtambikia

Bwana atakuumbia siku zote wingu

litakalokuwa lenye moshi la mchana

na lenye mwanga wa moto uwakao usiku,

kwani chote chenye utukufu hupaswa na kifuniko chake.

6Hivyo watapata pa kukalia kivulini mchana,

ukali wa jua usiwaumize,

tena pa kukimbilia na pa kujifichia,

kimbunga kisiwaangushe, wala mvua isiwapige.

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania