Mashangilio 114

Mashangilio 114

Nguvu za Mungu zilizowatoa Waisiraeli katika nchi ya Misri.

1Waisiraeli walipotoka kule Misri, wa mlango wa Yakobo walipotoka kwao wasemao msemo mgeni,[#2 Mose 12:41.]

2Ndipo, Yuda alipopata kuwa mwenye Patakatifu pao, naye Isiraeli mwenye ufalme wao.

3Bahari ilipoviona, ilikimbia, mto wa Yordani nao ukarudi nyuma.[#2 Mose 14:21-22; Yos. 3:13-16.]

4Milima ikarukaruka kama kondoo waume, navyo vilima vidogo kama wana wa kondoo.[#Sh. 68:9.]

5Wewe, bahari, ulionaje ulipokimbia? Wewe Yordani nawe, uliporudi nyuma?

6Nanyi milima, mliporukaruka kama kondoo waume? Nanyi vilima vidogo, mliporukaruka kama wana wa kondoo?

7Tetemeka, wewe nchi, Bwana akitokea, Mungu wake Yakobo akitokea mwenyewe![#2 Mose 19:18.]

8Anaugeuza mwamba kuwa ziwa la maji, nayo mawe magumu kuwa mboji za maji.[#2 Mose 17:6; 4 Mose 20:7-11.]

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania