Mashangilio 121

Mashangilio 121

Mchungaji mwelekevu wa Isiraeli.

1Ninayainua macho yangu na kuyaelekeza milimani, kwani ndiko, utakakotoka msaada wangu.[#Yes. 30:29.]

2Msaada wangu hutoka kwake Bwana, ndiye aliyeziumba mbingu na nchi.[#Sh. 124:8.]

3Hatautoa mguu wako, uje kujikwaa, maana halali usingizi akulindaye.

4Tazameni! Halali usingizi, wala hasinzii yeye aliye mlinzi wake Isiraeli.

5Bwana ndiye akulindaye, Bwana ni kivuli chako kuumeni kwako,

6mchana jua lisikuumize, wala mwezi usiku.

7Bwana atakukingia mabaya yote, atailinda roho yako.[#4 Mose 6:24.]

8Bwana na akulinde kutoka kwako na kuingia kwako kuanzia sasa hata kale na kale!

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania