Mashangilio 123

Mashangilio 123

Kumtazamia Mungu.

1Nimeyainua macho yangu na kuyaelekeza kwako, ukaaye mbinguni.

2Kama macho ya watumishi yanavyoitazama mikono ya bwana zao, au kama macho ya mjakazi yanavyoitazama mikono ya bibi yake, hivyo macho yetu humtazama Bwana Mungu wetu, hata atuhurumie.

3Tuhurumie, Bwana! Tuhurumie! Kwani tumeshiba sana mabezo.

4Roho zetu zimeshiba sana masimango yao wanaokula vya urembo, nayo mabezo yao wenye majivuno.

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania