The chat will start when you send the first message.
1Mwenye shangwe ni kila amwogopaye Bwana, azishikaye njia zake!
2Kwani utajilisha yayo hayo, mikono yako iliyoyasumbukia, kwa kuyapata hayo mema yako nawe u mwenye shangwe.
3Mke wako wa nyumbani mwako atafanana na mzabibu uzaao vizuri: watoto wako wataizunguka meza yako kama makuti ya mchikichi.[#Sh. 127:3.]
4Kwani ndivyo, mtu anavyobarikiwa akimwogopa Bwana.
5Bwana na akubariki toka Sioni, uyatazame mema ya Yerusalemu! Na uyaone na kuyafurahia siku zako zote za kuwapo,[#Sh. 134:3.]
6na uone nao watoto wa wanao! Utengemano na uwakalie Waisiraeli![#Sh. 125:5; Gal. 6:16.]