The chat will start when you send the first message.
1Bwana, yuko nani atakayetua hemani mwako? Yuko nani atakayekaa mlimani kwenye utukufu wako?[#Sh. 84:5.]
2Ni yeye ayendeleaye yaliyo sawa na kufanya yaongokayo, ni yeye awazaye moyoni mwake yaliyo kweli.[#Yes. 33:15.]
3Ulimi wake hausemi yaliyo masingizio; hamfanyizii mwenziwe kibaya, naye, waliyetua pamoja, hamtii soni.
4Aliyetupwa si kitu machoni pake, lakini wamchao Bwana anawaheshimu; kama ameapa, hageuzi, ijapo yampatie mabaya.
5Mali zake hazikopeshi, zimpatie faida nyingi, wala hatwai mapenyezo ya kumpatiliza asiyekosa. Aendeleaye hivyo hatatikisika kale na kale.[#2 Mose 22:25.]