The chat will start when you send the first message.
1*Bwana ni mchungaji wangu, hakuna nitakachokikosa.[#1 Mose 48:15; Yoh. 10:12-16.]
2Hunipumzisha mawandani penye majani mazuri, hunipeleka nako kwenye vijito, nipate kutua.[#Ez. 34:14; Ufu. 7:17.]
3Huutuliza moyo wangu kwa kuniongoza, nifuate mapito yaongokayo, Jina lake litukuzwe.[#Yer. 31:25.]
4Hata nitakapopita bondeni kwenye giza la kufa, siogopi kibaya, kwani huko nako wewe uko pamoja nami, fimbo yako na mkongojo wako utanishikiza.[#Sh. 46:3.]
5Wanitandikia meza machoni pao wanisongao, ukanipaka mafuta kichwani pangu, nacho kikombe changu hukijaza, mpaka kimwagikie.[#Sh. 36:9.]
6Kweli wema na upole utanifuata siku zote za kuwapo kwangu, nikae Nyumbani mwa Bwana siku zitakazokuwa zote.*[#Sh. 84:4-5; Rom. 8:31-39.]