Mashangilio 3

Mashangilio 3

Wimbo wa asubuhi wa kumtegemea Mungu.

1Bwana, tazama, jinsi walivyo wengi wanaonisonga! Tena ni wengi wanaoniinukia.[#2 Sam. 15:14.]

2Ndio wengi wanaoiwazia roho yangu ya kwamba: Hapana wokovu, atakaoupata kwake Mungu.

3Lakini wewe Bwana, u ngao inikingiayo, kwa kuwa utukufu wangu utakikweza kichwa changu.[#Sh. 84:12.]

4Ninapoipaza sauti yangu, ifike kwake Bwana, huniitikia toka mlimani kwenye utakatifu wake.

5Mimi nililala usingizi, kisha nikaamka, kwani mwenye kunishikiza ni Bwana.[#Sh. 4:8; Fano. 3:24.]

6Ijapo, watu wawe maelfu na maelfu, siwaogopi, wakija kunipangia na kunizunguka.[#Sh. 27:3.]

7Inuka, Bwana! Niokoe, Mungu wangu! Kwani walio adui zangu unawapiga makofi wote, ukawavunja meno wasiokucha, wewe.[#Sh. 58:7.]

8Kwako Bwana uko wokovu, uwapatie mema wao walio ukoo wako.[#Yer. 3:23.]

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania