Mashangilio 32

Mashangilio 32

Furaha ya kuondolewa makosa.

(Wimbo wa juto wa 2.)

1*Mwenye shangwe ndiye aondolewaye mapotovu, naye aliyefunikwa makosa yake.[#Rom. 4:6-9.]

2Mwenye shangwe ni mtu, Bwana asiyemhesabia manza, asiyekuwa na udanganyifu rohoni mwake.[#Luk. 18:13.]

3Kwani nilipoyanyamazia, mifupa yangu ikanyauka kwa hivyo, nilivyopiga kite mchana kutwa.[#Sh. 31:11; 51:10.]

4Kwani mkono wako ulinilemea mchana na usiku, kiini cha mifupa kikakauka kama maji penye kiangazi.

5Ndipo, nilipokuungamia makosa yangu, nazo manza, nilizozikora, sikuzifunika; nikasema: Nitamwungamia Bwana mapotovu yangu; ndipo, wewe uliponiondolea manza, nilizozikora kwa kukosa.[#Fano. 28:13.]

6Kwa hiyo kila akuchaye atakubembeleza, siku zitakapotimia; maji mengi yatakapofurika hayatamfikia.

7Wewe nidwe ficho langu, utanilinda, nisisongeke; utanipa, nikushangilie po pote kwa kuniponya.*

8Nitakufundisha na kukuonyesha njia, utakayoishika; macho yangu yatakuelekeza, nikikupa shauri.[#Sh. 25:12.]

9Msiwe kama farasi au nyumbu wakosao akili! Wasipotiwa hatamu na mafungo hawaji kwako.[#Fano. 26:3.]

10Maumivu yake asiyemcha Mungu ndiyo mengi, lakini amwegemeaye Bwana hugawiwa mengi, yamzunguke.

11Mfurahieni Bwana na kumshangilia, ninyi waongofu! Nyote mnyokao mioyo, pigeni vigelegele![#Sh. 33:1.]

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania