Mashangilio 61

Mashangilio 61

Kumwombea mfalme.

1Mungu, lisikie lalamiko langu!

2Yaitikie nikuombayo!

3Kwenye mapeo ya nchi ninakuita, moyo wangu ukizimia. Unikweze mwambani! Kwani ni mrefu wa kunishinda.

4Kwani kimbilio langu ndiwe wewe, u mnara wenye nguvu machoni pao adui.[#Sh. 18:2-3; 71:3.]

5Ninataka kuwamo katika kituo chako kale na kale, na kulikimbilia ficho lililomo mabawani mwako.[#Sh. 63:3.]

6Kwani wewe, Mungu, umeyasikia niliyokuapia, ukanigawia fungu lao waliogopao Jina lako.

7Unamwongezea mfalme siku kwa siku, miaka yake iwe ya vizazi na vizazi.[#Sh. 21:5.]

8Akiendelea machoni pake Mungu atakaa kale na kale. Agiza vya upole na vya kweli, vimsimamie![#2 Sam. 7:16.]

9Hivyo nitaliimbia Jina lako kale na kale na kuyalipa siku kwa siku niliyokuapia.

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania