Mashangilio 75

Mashangilio 75

Maamuzi yake Mungu ni ya kweli.

3Unasema: Itakapofika siku, niliyoiweka, mimi nitatoa maamuzi yanyokayo.

4Ijapo, nchi zitetemeke pamoja nao wazikaliao, mimi ndimi ninayezishikiza nguzo zake.

5*Niliwaambia wenye majivuno: Msijivune! Msielekeze mabaragumu juu, ninyi msionicha!

6Mabaragumu yenu msiyaelekeze juu kabisa, wala msinyoshe shingo mtakaposema!

7Kwani maawioni siko, wala machweoni siko, wala nyikani siko, ukuu utokako.

8Kwani Mungu ndiye anayeamua; yeye ndiye anayenyenyekeza, tena ndiye anayekweza.*[#1 Sam. 2:7.]

9Kwani mkononi mwake Bwana kimo kikombe kilichojaa mvinyo zichemkazo kwa viungo vikali, wote pia wasiomcha Mungu katika nchi huwagawia, wanywe, mpaka wafyonze mashimbi nayo.[#Sh. 60:5; Yer. 25:15-16.]

10Lakini mimi nitamtangaza kale na kale, Mungu wake Yakobo nitamwimbia sifa.

11Nayo mabaragumu yao wasiomcha Mungu nitayavunja yote, lakini mabaragumu yao wamchao yataelekezwa juu.

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania