The chat will start when you send the first message.
1Ni kitu kizuri kumshukuru Bwana na kuliimbia Jina lako, ulioko huko juu,[#Sh. 147:1.]
2asubuhi kuutangaza upole wako, tena usiku welekevu wako
3kwa kupiga mapango yenye nyuzi kumi pamoja na mazeze yaliayo vizuri.[#Sh. 33:2.]
4Kwani, wewe Bwana, umenifurahisha kwa matendo yako, kazi za mikono yako ninazishangilia.
5Kazi zako, Bwana, ni kubwa peke yao, mawazo yako ni marefu mno, hayachunguziki.[#Sh. 104:24; Yes. 55:9.]
6Lakini mtu asiyejua kitu hayatambui, wala mpumbavu hayaoni hayo.
7Wasiomcha Mungu wakichipuka kama majani, nao wote wafanyao maovu wakichanua vizuri, ni kwamba tu: Sharti waangamizwe kale na kale.[#Sh. 37:2.]
8Wewe, Bwana, unatukuka kale na kale.[#Sh. 97:9.]
9Kwani, Bwana, ukiwatazama wao wachukivu wako, ukiwatazama vema wao wachukivu wako, mara hupotea, wote wafanyao maovu hutawanyika.
10Lakini baragumu langu umelielekeza juu kama pembe za nyati, nikafurikiwa na mafuta ya mwaka huu.[#Sh. 23:5.]
11Macho yangu yataona furaha kwao walioninyatia, masikio yangu yatayasikia na kiyafurahia, wabaya walioniinukia waliyofanyiziwa.[#Sh. 91:8.]
12Mwongofu atachipuka kama mtende, atakua kama mwangati ulioko Libanoni.[#Sh. 52:10.]
13Kwenye Nyumba ya Bwana wako wlaiopandwa huko, watachipuza matawi katika nyua zake Mungu wetu;[#Sh. 84:3.]
14ijapo, wawe wazee, wataendelea kuzaa, maana watakuwa wenye utomvu na majani mengi.[#Sh. 1:3.]
15Hivyo watautangaza unyofu, Bwana alio nao; mwake yeye aliye mwamba wangu hamna upotovu.[#5 Mose 32:4.]