The chat will start when you send the first message.
1*Ndugu, moyo wangu unayapenda sana, ninayomwomba Mungu kwamba: Waisiraeli waokoke.
2Kwani nawashuhudia, ya kuwa waona wivu kwa ajili yake Mungu, lakini hawamtambui.
3Kwani wongofu, Mungu anaoutaka, hawaujui, wakajaribu kujiongoza wenyewe, lakini hivyo hawakuutii ule wongofu, Mungu anaoutaka.[#Rom. 9:31-32.]
4Kwani timilizo la Maonyo ni Kristo, kila mwenye kumtegemea ajipatie wongofu![#Mat. 5:17; Yoh. 1:17; 3:18; Gal. 3:24-25; Ebr. 8:13.]
5Kwani Mose aliandika:
Anayeufanya wongofu ulioagizwa na Maonyo
mtu huyo atapata uzima kwa njia hiyo.
6Lakini wongofu unaopatikana kwa kumtegemea Mungu unasema hivyo: Usiseme moyoni mwako: Yuko nani atakayepaa kwenda mbinguni? Huko ndiko kumshusha Kristo.[#5 Mose 30:12-13.]
7Wala usiseme: Yuko nani atakayeshuka kwenda kuzimuni? Huko ndiko kumpaza Kristo na kumtoa kwenye wafu.
8Tena unasema:
Neno hilo linakukalia karibu, limo kinywani mwako,
namo moyoni mwako.
Hilo ndilo neno la kumtegemea Mungu, ni hilihili, tunalolitangaza.
9Kwani ukiungama kwa kinywa chako kwamba: BWANA NI YESU, ukamtegemea kwa moyo wako kwamba: Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.[#2 Kor. 4:5.]
10Kwani ukimtegemea kwa moyo unapata wongofu; ukimwungama kwa kinywa unaokoka.
11Kwani Maandiko yasema: Kila anayemtegemea hatatwezeka.[#Yes. 28:16.]
12Kwani hapa hawachaguliwi Wayuda na Wagriki; kwani aliye Bwana wao wote ni yuyu huyu mmoja, ni mwenye magawio yanayowatoshea wote wanaomtambikia.[#Tume. 10:34; 15:9.]
13Kwani;
Kila atakayelitambikia Jina la Bwana ataokoka.
14Basi, watamtambikiaje, wasiyemtegemea? Tena watamtegemeaje, ambaye hawajamsikia Neno lake? Tena watasikiaje, pasipokuwapo mwenye kutangaza?
15Tena watatangazaje, wasipotumwa? Ndivyo ilivyoandikwa:
Tazameni, miguu yao wapiga mbiu njema jinsi inavyopendeza!*
16Lakini walioutii huo Utume mwema sio wote. Kwani Yesaya anasema:
Bwana, yuko nani anayeutegemea utume wetu?
17Basi, kumtegemea Mungu huletwa na matangazo, lakini matangazo hutoka katika Neno la Kristo.[#Yoh. 17:20.]
18Lakini niseme: Hawakusikia? Kusikia wamesikia.
Uvumi wao ulitokea katika nchi zote;
nayo maneno yao yalifika hata mapeoni kwa ulimwengu.
19Au niseme: Waisiraeli hawakulitambua? Kwanza Mose anasema:
Mimi na niwachokoze ninyi nikiwaletea watu wasio watu,
na niwakasirishe ninyi nikiwaletea taifa la watu
wasiojua maana.
20Kisha Yesaya anajipa moyo wa kusema:
Nimeonwa nao wasionitafuta, nikawatokea wasioniuliza.
21Lakini Waisiraeli anawaambia:
Mchana kutwa naliikunjua mikono yangu,
nipungie ukoo wa watu wasioonyeka, walio wabishi tu.