Zaburi 127

Zaburi 127

Baraka za Mungu nyumbani

1BWANA asipoijenga nyumba

Waijengao wanafanya kazi bure.

BWANA asipoulinda mji

Yeye aulindaye anakesha bure.

2Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema,[#Mwa 3:17]

Na kukawia kwenda kulala,

Na kula chakula cha taabu;

Yeye humpa mpenzi wake usingizi.

3Tazama, watoto ni urithi kutoka kwa BWANA,[#Mwa 33:5; Kum 28:4]

Uzao wa tumbo ni thawabu.

4Kama mishale mkononi mwa shujaa,

Ndivyo walivyo watoto wa ujanani.

5Heri mtu yule

Aliyelijaza podo lake hivyo.

Naam, hawataona aibu

Wanaposema na adui langoni.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya