Isaya 12

Isaya 12

Shukrani na sifa

1Na katika siku hiyo utasema,[#Isa 2:11; Zek 14:20,21]

Ee BWANA, nitakushukuru wewe;

Kwa kuwa ijapokuwa ulinikasirikia,

Hasira yako imegeukia mbali,

Nawe unanifariji moyo.

2Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu;[#Kut 15:2; Zab 118:14]

Nitatumaini wala sitaogopa;

Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu;

Naye amekuwa wokovu wangu.

3Basi, kwa furaha mtateka maji katika visima vya wokovu.[#Yer 2:13; Yn 4:10,14]

4Na katika siku hiyo mtasema,

Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake;

Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa,

Litangazeni jina lake kuwa limetukuka.

5Mwimbieni BWANA; kwa kuwa ametenda makuu;

Na yajulikane haya katika dunia yote.

6Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni;[#Isa 54:1; Sef 3:14; Lk 19:37-40]

Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya