The chat will start when you send the first message.
1Haleluya.[#111:1 maana yake ni, Msifuni BWANA.]
Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote,
Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano.
2Matendo ya BWANA ni makuu,[#Ayu 38:1]
Yafikiriwa sana na wapendezwao nayo.
3Kazi yake imejaa heshima na adhama,
Na haki yake yadumu milele.
4Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu;
BWANA ni mwenye fadhili na rehema.
5Amewapa wamchao chakula;
Atalikumbuka agano lake milele.
6Amewajulisha watu wake uwezo wa matendo yake,
Kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu,[#Zab 19:7]
Maagizo yake yote ni amini,
8Yamethibitika milele na milele,[#Ufu 15:3]
Yamefanywa kwa uaminifu na haki.
9Amewapelekea watu wake ukombozi,[#Ufu 15:3]
Ameamuru agano lake liwe la milele,
Jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10Kumcha BWANA ndio mwanzo wa hekima,[#Kum 4:6; Ayu 28:28; Mit 1:7; 9:10; Mhu 12:3]
Wote wafanyao hayo wana ufahamu mzuri,
Sifa zake zadumu milele.