The chat will start when you send the first message.
1Tuokoe, ee BWANA, maana hamna tena amchaye Mungu[#Isa 57:1]
Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu.
2Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe,
Wenye midomo ya kujipendekeza;
Husemezana kwa mioyo ya unafiki;
3BWANA ataikata midomo yote ya kujipendekeza,
Na ulimi unenao maneno ya kiburi;
4Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda;
Midomo yetu ni yetu wenyewe,
Ni nani aliye bwana juu yetu?
5Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge,[#Kut 3:7,8]
Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji,
Sasa nitasimama, asema BWANA,
Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.
6Maneno ya BWANA ni maneno safi,[#2 Sam 22:31; Zab 18:30; Mit 30:5]
Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi;
Iliyosafishwa mara saba.
7Wewe, BWANA, ndiwe utakayetuhifadhi,
Utatulinda na kizazi hiki milele.
8Wasio haki hutembea pande zote,
Huku ufisadi ukitukuka kati ya wanadamu.