Zaburi 121

Zaburi 121

Hakikisho la ulinzi wa Mungu

1Nayainua macho yangu niitazame milima,

Msaada wangu utatoka wapi?

2Msaada wangu hutoka kwa BWANA,

Aliyezifanya mbingu na nchi.

3Hatauacha mguu wako usogezwe;[#1 Sam 2:9; Isa 27:3]

Akulindaye hatasinzia;

4Naam, hatasinzia wala hatalala,

Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5BWANA ndiye mlinzi wako;

BWANA ni uvuli katika mkono wako wa kulia.

6Jua halitakupiga mchana,[#Isa 49:10]

Wala mwezi wakati wa usiku.

7BWANA atakulinda na mabaya yote,[#Ayu 5:19; Zab 91:9,10; Mit 12:21]

Atakulinda nafsi yako.

8BWANA atakulinda utokapo na uingiapo,[#Kum 28:6; Mit 2:8]

Tangu sasa na hata milele.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya